DB Troncatti yazidi kutesa BDL

TIMU ya DB Troncatti inaendelea kutesa katika ligi ya kikapu mkoa wa Dar es Salaam (BDL) upande wa  wanawake, ikionyesha ubabe kwa kuifunga timu DB Lioness kwa pointi 72-55.

Katika mchezo huo, DB Troncatti iliongoza katika robo ya kwanza  kwa pointi 19-12, 17-12, 22-16 na 14-15.

DB Troncatti  ilimaliza mzunguko wa kwanza kwa kutopoteza mechi hata moja ikionyesha kupania kulitwaa taji la michuano hiyo.

Katika ligi ya mwaka jana, timu hiyo ilishika nafasi ya mwisho, jambo ambalo ni tofauti na mwaka huu ambao ni wazi inaonekana imedhamiria kuwaziba midomo walikuwa wanaibeza.   

Hadi kufikia michezo 17 iliyocheza, DB Troncatti ilikuwa inaongoza kwa pointi 34, ikifuatiwa na Vijana Queens  yenye pointi 30.

Related Posts