MILIONI 177 ZATOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE,VIJANA NA WENYE ULEMAVU BUSOKELO

 

Na Mwandishi Wetu

HALMASHAURI ya Wilaya ya Busokelo imefanikiwa kutoa mikopo ya asilimia 10 kama takwa la kisheria na maelekezo Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. 
Akizungumza kuhusu mikopo hiyo Mkurugenzi wa  Halmashauri  hiyo Dkt.Mwinyi Omary Mwinyi amesema jumla ya Sh.milioni 177 zimetolewa kwa vikundi hivyo  Februari 6,2025 ikiwa ni awamu ya kwanza ya kutoa mikopo. 
Aidha  Dkt. Mwinyi ameeleza awamu ya pili imeanza kwa usaili wa vikundi mbalimbali kuanzia Februari 2 mpaka Februari 30 mwaka huu ambapo Sh.milioni 500 zinatarajiwa kutolewa kwa vikundi vitakavyopitishwa.

 

Related Posts