-Atakagua na Kuzindua Miradi ya Maendeleo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu -Mhe. Ridhiwani Kikwete leo Februari 23, 2025 amewasili mkoani Songwe kwa lengo la ziara ya kukagua miradi ya Maendeleo ikiwemo ya sekta ya Elimu, Afya na Miundombinu kwa ajili ya ustawi wa maendeleo ya wananchi .
Mhe. Waziri Kikwete anatarajiwa kukagua na kuweka Mawe ya msingi katika miradi hiyo ambayo inakadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 700 katika Halmashauri zote za mkoa huo.
Mara baada ya kuwasili katika mkoa huo, Waziri Kikwete alipokelewa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Daniel Chongolo ambaye alimpa hali ya maendeleo ya Mkoa huo na maandalizi ambayo yameshafikiwa kwa ajili ya ziara hiyo.
Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Kikwete ameambatana na watendaji mbalimbali ambapo amemhakikishia Mkuu wa mkoa huo kuwa timu yake iko tayari kwa ajili ya kazi iliyowaleta.
Vile vile, Mhe. Kikwete anatarajiwa pia kukagua Maendeleo ya Kituo cha Vijana cha Sasanda kilichopo wilayani Songwe ambapo atakagua mradi wa Shamba la vijana lililopo katika kituo hicho.