Benki ya Absa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya wanawake mahali pa kazi

Na mwandishi wetu.

Benki ya Absa Tanzania imesema itaendelea kuunga mkono juhudi mbalimbali zenye lengo la kuhakikisha wanawake wa Tanzania wanapiga hatua za kimaendeleo mahali pa kazi.

 Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser, jijini Dar es Salaam hivi karibuni, wakati wa maadhimisho ya miaka 10 na mahafali ya 10 ya programu ya Mwanamke Kiongozi, inayoratibiwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE).

 “Sisi Absa tuna kitu tunaita ahadi yetu ya chapa inayosema ‘Stori yako ina thamani’, kwa kuendana na ahadi yetu hii tunaamini kwamba story za wanawake wa Tanzania zina thamani na ndio maana tuliamua kuungana na ATE kusapoti jambo ili kama wadhamini , lakini pia tumekua wadau wa karibu sana na ATE kwa miaka 10 tumeweza kuweka wahitimu wengi, leo hii tukiwa na wahitimu kama wanne.

 “Sababu kubwa inayotufanya tuendelee kusapoti juhudi hizi ni kwamba kwenye miaka hivi karibuni tumekuwa na mafanikio makubwa sana katika utendaji, wale ambao mnafuatilia nadhani mtakuwa mashahidi na sababu kubwa ya kwanini tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa ni kwa sababu tumekuwa na viongozi wanawake kwenye timu ya uongozi.

 “Sisi Absa, tuna idara mbalimbali, tuna idara nne za biashara, kati ya hizo, tatu zinaongozwa na wakurugenzi wanawake, wamepata promosheni hivi karibuni kuingia katika ngazi ya ukurugenzi, hawa ndio wakurugenzi wa biashara, hivyo basi mafanikio ya benki yetu hayawezi kabisa kutenganishwa na uwepo wa viongozi wanawake”, alisema Bw. Laiser.

 Mmoja wa wahitimu wa programu hiyo, kutoka Benki ya Absa, Ikunda Kishimbo, ambayo tokea ianzishwe jumla ya washiriki 462 kutoka sekta binafsi na umma wamehitimu alisema, programu hiyo imewajengea washiriki kujiamini na kuwapa uwezo wa kiutendaji katika maeneo yao ya kazi.

 Mafunzo yanayotolewa kupitia Programu ya Mwanamke Kiongozi pamoja na kuwa na lengo la kuongeza ujuzi wa wanawake viongozi, lakini pia yanasaidia kuongeza msukumo wa suala la usawa wa kijinsia katika mahali pa kazi.Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza machache kuhusu huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na benki hiyo, wakati wa maadhimisho na mahafali ya 10 ya Programu ya Mwanamke Kiongozi inayoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.Baadhi ya wahitimu wa Programu ya Mwanamke Kiongozi inayoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) kutoka Benki ya Absa Tanzania, Ikunda Kishimbo na Vailet Ephata,  wakipozi kwa picha katika hafla ya maadhimisho na mahafali ya 10 ya programu hiyo, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete (kushoto), akikabidhi cheti Kwa Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdau muhimu wa Programu  ya Mwanamke Kiongozi inayoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), katika hafla ya maadhimisho na mahafali ya 10 ya programu hiyo, jijini Dar es Salaam, hivi karibuni.Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Samia Suluhu Hassan (katikati), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Ridhiwani Kikwete (kulia kwake), wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na wadhamini na viongozi mbalimbali, muda mfupi mara baada ya kukamilika kwa hafla ya maadhimisho na mahafali ya 10 ya Programu ya Mwanamke Kiongozi iliyoratibiwa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Related Posts