Bosi Azam FC Afungukia Kuhusu Fei Toto – Global Publishers


FEISAL Salum, Fei Toto kiungo wa Azam FC

FEISAL Salum, Fei Toto kiungo wa Azam FC ambaye ni namba moja kwenye pasi za mwisho za mabao ndani ya Ligi Kuu Bara ambayo ni namba nne kwa ubora jina lake limekuwa likitajwa kuwa katika rada za Simba.

Kiungo huyo aliibuka ndani ya Azam FC akitokea Yanga ambapo kwa sasa amekuwa ni chaguo la kwanza kwenye viunga vya Azam Complex akiwa ametoa jumla ya pasi 12 za mabao kati ya 36 yalyofungwa na timu hiyo.

Nafasi ya tatu kwenye msimamo ipo baada ya kucheza mechi 23 kibindoni ina pointi 48 vinara ni Yanga wenye pointi 58 na Simba inayotajwa kuwa kwenye hesabu za kuisaka saini ya Fei Toto ni nafasi ya pili na pointi 57.

Ikumbukwe kwamba baada ya mchezo wa Mzizima Dabi uliochezwa Uwanja wa Mkapa ubao uliposoma Simba 2-2 Azam FC, Fei Toto alivaa uzi wa Simba walipobadilishana na mchezaji Shomari Kapombe jambo ambalo liliongeza gumzo.

Kuhusu Sakata hilo, Mkuu wa Idara ya Habari ndani ya Azam FC, Zakazakazi amesema kuwa ilikuwa ni gumzo kubwa kwa Fei Toto kutokana na thamani yake kuwa kubwa jambo ambalo linaleta gumzo.

“Kwa Fei Toto kuvaa jezi ya Simba baada ya mchezo hiyo ilikuwa ni stori kubwa kutokana na thamani ya mchezaji, akifanya kitu chochote kinapoteza yote yaliyokuwa yanafanyika awali kutokana na uwezo wake ila bado atabaki kuwa mchezaji wetu.”

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu usipange kukosa.

Related Posts