Mhandisi Mwandamizi wa Maji na Usafi wa Mazingira Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Amani Nyekele akiwapitisha washiriki wa mkutano katika vipengele vya Kanuni vinavyopendekezwa kuboreshwa, wakati wa mkutano wa EWURA na Watendaji wa Mamlaka za Maji nchini jijjni Dar es Salaam leo 20 Machi 2025
Na.Mwandishi Wetu-Dar es Salaam:
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) leo, 21 Machi 2015, imekutana na watendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira nchini kwa lengo la kupokea na kujadili maoni kuhusu maboresho ya Kanuni za Ubora wa Huduma ya Maji ili kuongeza ufanisi kwa Mamlaka hizo katika kuwahudumia wateja wake.
Mkurugenzi wa Maji na Usafi wa Mazingira EWURA, Mhandisi Exaudi Maro, alibainisha kuwa baadhi ya maboresho ya Kanuni hizo ni pamoja na mapendekezo ya kuongezeka muda wa kutumika bei za maji kutoka miaka mitatu ya sasa hadi mitano, kuboresha muda wa kuwasilisha taarifa za utendaji, na kuweka ukomo wa mipango ya kibiashara ya mamlaka za maji.
Sabina Faya, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mha. Mwajuma Waziri, aliwasisitiza washiriki kutoa maoni yenye tija ili yawe na matokeo chanya katika kuboresha huduma na kuongeza ufanisi wa huduma ya maji kwa wateja nchini.
Mkurugenzi wa Maji na Usafi wa Mazingira Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mhandisi Exaudi Maro,akizungumza wakati wa Mkutano wa wadau wa Mamlaka za Maji uliondaliwa na EWURA kujadili maboresho ya Kanuni za Utoaji huduma za maji nchini,leo Machi 20,2025 jijini Dar es Salaam.
Sehemua ya washiriki kutoka Mamlaka za Maji wakifatilia mkutano wa wadau uliondaliwa na EWURA kujadili maboresho ya Kanuni za Utoaji huduma za maji nchini,leo Machi 20,2025 jijini Dar es Salaam.
Sehemua ya washiriki kutoka Mamlaka za Maji wakifatilia mkutano wa wadau uliondaliwa na EWURA kujadili maboresho ya Kanuni za Utoaji huduma za maji nchini,leo Machi 20,2025 jijini Dar es Salaam.