Namba zaipa Simba bao 2 dhidi ya Al Masry

SIMBA ina deni la kurudisha mabao mawili kisha kusaka la ushindi itakapocheza dhidi ya Al Masry ili kufuzu nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Hiyo inatokana na kipigo cha mabao 2-0 ilichokubali ugenini katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya michuano hiyo uliochezwa Jumatano iliyopita nchini Misri.

Kuelekea mchezo huo wa marudiano utakaofanyika Jumatano ijayo kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, takwimu zinaonekana kuibeba Simba katika suala zima la kufunga mabao mawili uwanja wa nyumbani, huku ikiwa na mtihani wa kuwazuia wapinzani wao Al Masry wasifunge kwani nao wana wastani wa kufunga bao moja kwa mechi za ugenini.

Related Posts