Namba zamkatisha tamaa Kocha Azam

KIPIGO cha bao 1-0 ilichokipata Azam mbele ya Singida Black Stars, kimemfanya kocha wa timu hiyo, Rachid Taoussi kuonyesha dalili za waziwazi amekata tamaa.

Azam kwa sasa ipo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 51 baada ya kucheza mechi 25 na Taoussi alisema matumaini ya wao kutwaa ubingwa msimu huu yamevunjika huku akiitaja Yanga kushika hatma yao kuendelea kusalia nafasi waliyopo sasa.

Tofauti yao na vinara Yanga ni pointi 10 kabla ya mchezo wa jana.

Akizungumza na Mwanaspoti, Taoussi alisema; “Sio rahisi kushinda mechi zote, tuna uwezo wa kumfunga kila mpinzani anayekuja mbele yetu, lakini kuna wakati tukubali hatuwezi kushinda kwa kila mechi. Tunahitaji umakini zaidi katika mechi zijazo kwa sababu hakuna mchezo utakaouwa rahisi.”

Related Posts