NA VICTOR MASANGU,PWANI
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha mapinduzi (CCM) Taifa Taifa Hamoud Juma (MNEC) kupitia wazazi katika juhudi za kukiimarisha chama ameahidi kuchangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa jumuiya wa wazazi Wilaya ya Kibaha mjini.
Juma ametoa ahadi hiyo wakati alipokuwa mgeni rasmi katika kufunga rasmi kikao cha baraza la jumuiya ya wazazi Wilaya ya Kibaha mjini kilichohudhuliwa na viongozi mbali mbali wa chama cha mapinduzi (CCM) pamoja na jumuiya zake sambamba kwa lengo la kuweza kubadilishana mawazo na kuweza kuweka mikakati kabambe ya kuimarisha na kuijenga jumuiya hiyo kuanzia ngazi za chini.
Alisema kwamba lengo lake lake kubwa ni kuhakikisha kwamba anashirikiana bega kwa bega na jumuiya ya wazazi ndio maana ameamua kuchangia mifuko 100 ya saruji ambayo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa nyumba ya mtumishi na kwamba ataendelea kuwapa sapoti katika mambo mbali mbali ya kimaendeleo.
“Kwa upande wangu mimi nimefarijika sana kuweza kunialika katika kikao cha baraza kuna mambo mengi ambayo mmeyasema na mimi kwa kushirikian na wenzangu tutaona namna ya kufanya ili lakini mimi katika kuwaunga mono nitachangia mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mtumishi kwani hii ni moja ya hatua kubwa katika kuimarisha jumuiya yetu ya mtumishi kuwa na nyumba ikiwa saambamba na kuitangaza jumuiya yetu,”alisema Juma.
Pia alimpongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuteuliwa na mkutano mkuu maalumu kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Urais pamoja na mgombea mwenza Dkt. Emmanuel Nchimbi kwani wajumbe wamemekuwa na imani nao kubwa katika katika uchaguzi mkuuu wa mwaka wa 2025.
Aidha Juma ameitaka jumuiya ya wazazi kuhakikisha kwamba wanakuwa na umoja na mshikamano sapoti ya kutosha viongozi waliopo madarakani wakiwemo madiwani, pamoja na wabunge wafanya kazi zao katika kutekeleza ilani ya chama mpaka hapo muda wao utakapofika na sio kuanza kuwaingilia katika majukumu yao.
Katika hatua nyingine katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 amewahimiza wagombea wote katika nafasi za udiwani na ubunge kuhakikisha kwamba wanaheshimu kauli ya Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kukemea vikali vitendo vya kufanya kampeni za chini chini kabla ya muda wake kwani ni kinyume kabisa na utaratibu wa chama cha mapinduzi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Wilaya ya Kibaha mjini Yahaya Mtonda ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo yote ambayo wamepatiwa na kwamba atahakikisha wanajipanga imara kuanzia ngazi za chini kwa ajili ya kumpa sapoti kubwa Rais Samia Suluhu pamoja na mgombea mwenza ili waweze kushinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025.