KUMBILAMOTO AWATAKA WAKANDARASI KUKAMILISHA MIRADI KWA WAKATI

 

 Na Humphrey Shao, Michuzi Tv

Wito umetolewa kwa wakandarasi kukamilisha kazi kwa wakati hili kutoa taswira ya hali ya fedha zinazotolewa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa wanachi wake.

Wito huo umetolewa leo na  Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar-es-Salaam Omary Kumbilamoto  akiwa katika ziara yake ya kutembelea miradi iliyokuwa imekwama na sasa imekwamuliwa  na kupewa wakandarasi wengine, ambapo leo ametembelea  Kata ya Majohe Mtaa Viwege kukagua Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya chenye Thamani ya Tsh. million 500.

” pesa hizi zimetolewa na  Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na sisi Halmashauri tumepewa dhamana ya kuwa wasimamizi hivyo atuwezi kukubali sisi tuonekane kikwazo cha kuwa ndio tunamkwamisha Rais wakati nyie mmepewa kila kitu ambacho kinawezesha mradi huu kukamilika” amesema Kubilamoto.

 Kumbilamoto  amesema kuwa ifike mwisho wa wakandarasi au mafundi waliopewa kazi kufanya kazi kwa mazoea  na kupelekea hasara kwa serikali kwani sisi kama halmashauri tumejifunza na atutacheka na mzembe yoyote aliyepanga  kuja kutukwamisha.

katika ziara hiyo  mstahiki meya Kumbilamoto alipata kuongozana na  Diwani wa Kata ya Majohe Pascal Linyamala na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Kata ya Majohe Nuru Mizumo na Katibu wa CCM Kata ya Majohe Ndg. Pius Kagete wote kwa pamoja walitoa Shukrani kwa Mstahiki Meya  kwa kufanya ziara ya kukagua ujenzi wa kituo hicho, ambacho kilisimama kwa muda mrefu bila Muendelezo na huku wananchi wakiendelea kuteseka na kumuomba awafikishie salamu za shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan.

Related Posts