BDL sasa kufanyika Aprili | Mwanaspoti

Kamishina wa ufundi na mashindano wa Ligi ya kikapu mkoa wa Dar es Salam (BDL), Haleluya Kavalambi amesema ligi hiyo inatarajiwa   kuanza mwezi Aprili na tarehe kamili itatangazwa  baada ya kikao cha kwanza  cha BD  na klabu kufanyika. 

“Kikao hicho kitazungumzia mapitio ya kanuni  na kuzipitisha, ambazo ndizo zitakazoongoza na kusimamia msimu wa Ligi  ya 2025,” alisema Kavalambi.

Alitaja timu zitakazoshiriki  upande wanaume ni JKT, UDSM Outsiders, Dar City, ABC, Chui, DB Oratory, KIUT, Mgulani JKT, Vijana ‘City Bulls’, Srelio, Savio, Mchenga Star, Pazi, Polisi, Stein Warriors na Kurasini Heat.

Kwa upande wa timu za wanawake ni DB Lioness, Vijana Queens, JKT Stars, Jeshi Stars, Polisi Stars, Tausi Royals, UDSM Queens, DB Troncatti, Pazi Queens na Twalipo Queens.

“Timu za wanawake ambazo, zinataka kushiriki ligi ya mkoa wa Dar es Salaam, zinatakiwa kutuma uthibitisho  kwa maandishi  na kuwasilisha barua kwa mkurugenzi wa ufundi na mashindano wa BD,” alisema Kavalambi.

Related Posts