UHURU USIO NA MIPAKA NI FUJO-PROF. KABUDI.

…………….

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi  amesema 

Vyombo vya habari vimechangia katika utekelezaji wa 4R za Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwakuwa  ni sekta muhimu katika kupeleka ujumbe kwa jamii.

Aidha, Prof. Kabudi  amewataka Wanahabari kufanyakazi kwa kuzingatia maadili , Uhuru  na taratibu za taaluma hiyo ili kupunguza  changamoto zinaweza kujitokeza katika jamii kutokana na mgongano wa kimaslahi 

Prof. Kabudi ameyasema hayo leo Jumatatu Aprili 14,2025 Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu   mafanikio na mwelekeo wa  Wizara hiyo   katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Sambamba na hilo ameongeza kuwa Wizara imefanikiwa kuleta utulivu kwenye sekta ya habari ambapo vyombo vya habari vilivyokuwa vimefungiwa kwa Makosa  mbalimbali vilifunguliwa na Wizara imekuwa na mweleke wa kuvilinda vyombo vya habari Hali iliyosababisha kuogezeka kwa uhutru  wa vyombo vya habari.

Waziri Kabudi amesisitiza kuwa uhuru  wowote una mipaka hakuna uhuru  ambao hauna mipaka kwani Uhuru  ambao hauna mipaka ni fujo.

 

Related Posts